JKU NA MIEMBENI CITY SEPTEMBA 19 NGAO YA JAMII AMAAN


Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka ya Zanzibar timu ya JKU, pamoja na mabingwa wa ligi daraja la kwanza Taifa timu ya Miembeni City watakutana Jumanne Septemba 19, mwaka huu kwenye Uwanja wa Amaan katika mchezo wa Ngao ya Jamii kuashiria kufunguliwa kwa pazia la Ligi Kuu soka Visiwani Zanzibar mchezo ambao utapigwa majira ya saa 10:00 za jioni.


Mjumbe wa ZFA Taifa kutoka Wilaya ya Mjini
Abdul-Wahab Dau Haji ameuambia Mtandao huu kwamba, Ligi Kuu yenyewe itaanza rasmi Oktoba 3, 2017 na mchezo wa ngao utapigwa Septemba 19, 2017.

Amesema wanacheza JKU na Miembeni City kwa kuwa ndio wenye sifa ya kucheza mchezo wa Ngao kutokana na kufanya vyema msimu uliopita katika madaraja yao.

“Mchezo wa Ngao utachezwa Jumanne ijayo kati ya Miembeni city na JKU, huu ni mchezo wa kufungua ligi kuu ya Zanzibar, JKU ni Bingwa wa ligi kuu na City ni Bingwa wa daraja la kwanza hivyo lazima wacheze wao Ngao”. Alisema Dau.


Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE