KOMBE LA MTOANO KUENDELEA KESHO KUTWA JUMANNE, JUMATANO SAILORS NA POLISI

Kesho kutwa Jumanne ya Septemba 5, 2017 kutapigwa michezo miwili ya Kombe la Mtoano yaloandaliwa na chama cha Soka Wilaya ya Mjini kati ya Mwembe makumbi dhidi ya Raska zone city saa 8:00 za mchana , na saa 10:00 jioni Kundemba itacheza na El Hilal, michezo yote katika uwanja wa Amaan.

Siku ya Jumatano kutakuwa na shughuli pevu kati ya Polisi na Black Sailors timu zote hizo zinacheza ligi kuu soka ya Zanzibar mchezo ambao utapigwa saa 10:00 za jioni katika uwanja wa Amaan.

Mpaka sasa timu 4 tayari zimeshatinga hatua ya robo fainali kufuatia kushinda michezo yao ya awali ambazo ni Polisi Bridge, Negro United, Hawai na Shaba.

Mashindano hayo yameshirikisha vilabu vya madaraja tofauti vikiwemo vya ligi kuu soka ya Zanzibar, Daraja la Kwanza Taifa, Daraja la Pili Taifa, Daraja la Pili Wilaya na Daraja la Tatu.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE