UJAMAA NA POLISI ZATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA MTOAN

Kikosi cha Polisi 

Timu za Ujamaa na Polisi zimefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali kwenye Kombe la Mtoano linaloendelea kwenye Dimba la Amaan.

Polisi wamewatoa El Hilal kwa penalti 5-4 baada ya kutoka sare ya bao 1-1 kwenye dakika ya 90 ya mchezo huo uliopigwa saa 10 za jioni jana.

Bao la Polisi limefungwa na Mohd Hassan dakika ya 16 huku bao la El Hilal wakisawazisha dakika ya 86 kupitia Juma Makame.

Na wakati wa saa 8 za mchana Ujamaa Sports Club wakaitoa Raskazone kwa kuifunga bao 1-0 kwenye mchezo huo.

Kwa matokeo hayo Polisi na Ujamaa wataungana na Shaba pamoja na Hawai kucheza hatua ya nusu fainali kwenye mashindano hayo ambapo bado haijajulikana lini na nani atacheza na nani.
Mashindano hayo yameandaliwa na Chama cha Soka cha Wilaya ya Mjini ambapo yalishirikisha vilabu 16 kwa madaraja tofauti vikiwemo vya ligi kuu soka ya Zanzibar, Daraja la Kwanza Taifa, Daraja la Pili Taifa, Daraja la Pili Wilaya na Daraja la Tatu .

 
Kikosi cha Ujamaa

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE