AZIZ SHAWEJI ASIMAMISHWA MECHI 4 KUCHEZA LIGI KUU ZENJ NA KOCHA ABRAHMAN MUSSA NAE APIGWA STOP KUKAA KATIKA BENCHI


Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) kimempa adhabu ya kumsimamisha kucheza mechi nne beki wa Kilimani City, Aziz Shaweji baada kupatikana na hatia ya kukiuka nidhamu ya michezo katika mechi kati ya Kilimani City na Black Sailors iliyopigwa juzi Jumapili saa 8 za mchana katika uwanja wa Amaan.

Akizungumzia kadhia hiyo katibu mkuu wa ZFA Mohd Ali Hilali “Tedy” amesema Shaweji alipatikana na kosa wakati timu yake ya Kilimani City ilipofungwa 2-0 na Black Sailors ambapo alimzonga Muamuzi wa kati wa mchezo huo Mfaume Ali Nassor.

Hivyo Shaweji atazikosa mechi kati ya Kilimani City dhidi ya Jang’ombe Boys itakayopigwa Oktoba 30, Kilimani city na Chuoni ya Novemba 6, Kilimani city dhidi ya Charawe ya Novemba 12 na ya mwisho Kilimani city dhidi ya Zimamoto itakayopigwa Novemba 19.

Wakati huo huo kocha wa Kilimani City Abrahman Mussa nae amesimamishwa kukaa katika benchi hadi pale atakapopeleka vyeti vyake vya ukocha ZFA.

Katibu Tedy amesema wamemsimamisha mpaka wathibitishe cheti chake cha ukocha kama kweli anastahiki kuwa Mwalimu wa Soka kwani katika mchezo kati Kilimani City walipochapwa 2-0 na Black Sailors uliyopigwa juzi Jumapili saa 8 za mchana katika uwanja wa Amaan Mwalimu huyo baada ya kumaliza mchezo alimzonga Muamuzi wa kati wa mchezo huo Mfaume Ali Nassor.
Kocha Abrahman Mussa Kushoto



Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS