JAN'GOMBE BOYS HOI KWA BLACK SAILORS

Mzunguko wa pili wa ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja umemalizika jioni ya leo ambapo timu ya Black Sailors (Mabaharia Weusi) wameichapa Jang’ombe Boys bao 1-0 kwenye mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Amaan.

Bao pekee la Sailors lililopeleka furaha kwa kocha wao Juma Awadh limefungwa na Abbas Peter John dakika ya 75 ya mchezo huo.


Mzunguko wa tatu wa ligi hiyo utaanza Jumamosi ya Oktoba 21 saa 8:00 za mchana katika uwanja wa Amaan kati ya Mafunzo na Taifa ya Jang’ombe na saa 10:00 za jioni kati ya JKU na Miembeni City.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE