LIGI KUU ZENJ YAANZA KWA KISHINDO , JKU RAHA RAHA, BOYS NA KMKM HAKUNA MBABE

Ligi kuu soka Visiwani Zanzibar kanda ya Unguja imeanza rasmi leo kwa kupigwa michezo miwili katika uwanja wa Amaan.

Mapema saa 8 za mchana Mabingwa watetezi wa ligi hiyo JKU wameanza vyema baada ya kuichapa Mafunzo bao 1-0 kwa bao lililofungwa na Ali Haji Said (Zege) dakika ya 44.

Mchezo mwengine uliopigwa kiwanjani hapo majira ya saa 10 za jioni Jangombe boys na KMKM wakaenda sare ya kufungana bao 1-1.

KMKM ndio wa kwanza kufunga bao kupitia Salum Akida dakika ya 5 ambapo bao la Boys lilifungwa na Khamis Mussa (Rais) dakika ya 25.


Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa kupigwa michezo miwili katika uwanja wa Amaan, saa 8:00 za mchana Kilimani City watasukumana na Kipanga, na saa 10:00 za jioni Charawe na Maafande wa KVZ.
Kikosi cha Jang'ombe Boys

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE