MWANARIADHA GULAM KWENDA BRUNEI KUFANYA MAZOEZI MIEZI 6

Ali Khamis Gulam
Chama cha Riadha Zanzibar (ZAA) kimepokea Visa ya Mwanariadha Ali Khamis Gulam ambae anatakiwa kwenda Brunei kufanya mazoezi kwa muda wa Miezi sita.

Akithibitisha kupokea Visa ya Mwanariadha huyo Mwenyekiti wa Chama cha Riadha Zanzibar Abdulhakim Cosmas Chasama amesema chao chao kimepokea Visa ya Gulam ambapo Visa hiyo inaaisha Januari 15, 2018.

“Tumepokea Visa ya Mwanariadha Ali Khamis Gulam kwenda Brunei kwaajili ya mazoezi miezi sita, atakwenda kule kwaajili ya mazoezi ili afikie viwango kwaajili ya kushiriki Mashindano ya Jumuiya ya Madola pamoja na Olimpik, tunawaomba wadau mbali mbali waweze kumsaidia kijana huyu ili aweze kusafiri, huduma za kule watamuhudumia wenyewe, sisi tunaombwa tumsafirishe, kwaiyo tiketi ni kazi yetu kuomba ili tusaidiwe mana visa yake inaisha Januari 15, 2018”. Alisema Chasama.

Mtandao huu umemtafuta Mwanariadha Gulam ambapo amesema amepokea kwa furaha taarifa hizo kwenda Brunei ambapo amewaahidi Wazanzibar kuyatumia vyema mazoezi hayo.

“Nimepokea taarifa hizi kwa furaha sana, nilijitahidi ndio mana nkapata nafasi hii, nawaahidi Wazanzibar na Watanzania kwa ujumla ntaenda kuyatumia vyema Mazoezi hayo ili niweze kufanya vyema katika Mashindano ya Jumuiya ya Madola”. Alisema Gulam. 



Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE