SIMBA WAANZA RASMI KUWATAFUTIA DAWA YANGA BAADA YA KUWASILI ZANZIBAR, WAPIGA MTIZI JESHINI
Kikosi
cha Simba kimeanza mazoezi mepesi jioni ya leo katika uwanja wa Jeshini
Migombani Mjini Unguja ambapo wapo Kisiwani hapa kwaajili ya Kambi maalum
kujiandaa na mchezo wa ligi kuu soka ya Tanzania bara dhidi ya Watani wao Yanga
utakaopigwa Oktoba 28, 2017 katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es salam.
Jumla
ya wachezaji 24 wa Simba pamoja na viongozi wao wamewasili Unguja asubuhi ya leo
wakitokea Jijini Dar es salam kwa furaha baada ya Jumamosi iliyopita kuwachapa
4-0 Njombe Mji kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Simba
wataendelea kufanya mazoezi kila siku asubuhi kuanzia saa 3:00 katika uwanja wa
Amaan na saa 10:00 za jioni katika uwanja wa Jeshini Migombani.
Kikosi
hicho kinachonolewa na Mkameroon Joseph Omog pamoja na msaidizi wake mpya
Mburundi Masoud Djuma
Irambona kimefikia kwenye Hoteli ya Mtoni Marine
iliyopo Maruhubi Mjini Unguja.
Comments
Post a Comment