ZEGE AWEKA RIKODI KUBWA LIGI KUU ZENJ

Ukiwa ni msimu wake wa kwanza katika Ligi Kuu Soka Zanzibar Kanda ya Unguja, mshambuliaji wa klabu ya JKU Ali Haji Said (Zege) ameweka rikodi ya kufunga bao la mwanzo kwenye ligi hiyo timu yake ikiibuka na ushindi wa bao 1-0 mchezo uliopigwa katika uwanja wa Amaan.

Nyota huyo alifunga bao la kwanza la msimu huu wa 2017/2018 katika dakika ya 44 pambano dhidi ya Mafunzo kabla ya wachezaji wengine hawajaanza kuandika mabao katika michezo mengine ilifuata.

Mshambuliaji huyo ambaye amesajiliwa na JKU kutoka JKT Ruvu Tanzania bara ilimchua dakika 44 tu kuonyesha thamani yake ndani ya JKU.
Mara baada ya kuweka rikodi hiyo Zege amefurahishwa mno mechi yake ya kwanza kufunga bao katika ligi hiyo.

“Nimefurahi sana kufunga bao, mechi yangu ya kwanza kisha nimeweka rikodi ya kufunga bao la mwanzo, kwangu mimi ni faraja sana, wapenzi wa JKU wategemee mazuri kutoka kwangu, kwasababu tuna umoja na upendo katika kikosi chetu cha JKU”. Alisema Zege.

Katika msimu uliopita bao la kwanza lilifungwa na mchezaji wa Mundu, Mwinyi Mbegu ndani ya dakika ya 22 katika pambano dhidi ya Kimbunga ambapo Mundu ilishinda mabao 2-1 ilikuwa 02/10/2016 katika uwanja wa Amaan.


Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE