ZIMAMOTO YAENDELEA KUVUTWA SHATI, KVZ YAREJEA KILELENI



Ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja imeendelea tena leo kwa kupigwa michezo miwili katika uwanja wa Amaan ambapo saa 8 za mchana Zimamoto na Kipanga zilishindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya kufungana bao 1-1.

Bao la Kipanga limefungwa na Nassor Ali wakati bao la Zimamoto likiwekwa nyavuni na Hassan Haji.

Saa 10 za jioni katika uwanja huo KVZ wakaitandika Polisi bao 1-0 kwa lililofungwa na Salum Songoro dakika ya 79.

Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa kupigwa mchezo mmoja katika uwanja wa Amaan saa 10:00 za jioni kati ya Jang’ombe boys dhidi ya Chuoni.
 
Zimamoto

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE