ZIMAMOTO YAPIGWA NNE,SONGORO APIGA HAT-TRICK YA KWANZA MSIMU HUU ZENJ



Mshambuliaji wa KVZ Salum Songoro amefungua ukurasa mpya ligi kuu soka ya Zanzibar msimu huu baada kufunga hat-trick ya kwanza katika ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Zimamoto mchezo uliopigwa jioni ya leo katika uwanja wa Amaan.

Songoro alifunga bao hizo katika dakika ya 9, 16 na 42, Sultan Juma Kaskas alifunga bao la nne katika dakika ya 61 huku mabao ya Zimamoto yalifungwa na Nyange Othman Denge dakika ya 63 na Idrissa Simai dakika ya 88.

Mapema saa 8 za mchana Taifa ya Jang’ombe na Polisi walishindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya 0-0 katika uwanja wa Amaan.

ligi hiyo itaendelea tena kesho Jumanne 17/10/2017 saa 8:00 za mchana Kipanga vs Charawe na saa 10:00 za jioni KMKM vs Kilimani City.

Jumatano 18/10/2017 saa 10:00 za jioni Black Sailors vs Jang’ombe Boys.
 
Mkurugenzi wa Ufundi wa ZFA Abdughan Msoma (Kulia) akimkabidhi Mpira Salum Songora wa KVZ baada ya kupiga Hat trick

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE