AMOUR PWINA AIBEBA ZANZIBAR HEROES

Timu ya Taifa ya Soka ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) imeendelea kucheza michezo ya kirafiki ambapo leo imefanikiwa kupata ushindi wa mabao 2-0 baada ya kuifunga timu ya Kombain iliochaguliwa na Makocha wa Zanzibar, mchezo wa kirafiki uliopigwa saa10 jioni katika uwanja wa Amaan.

Mabao ya Heroes yote yamefungwa na Amour Suleiman (Pwina) dakika ya 35 na 80 ya mchezo.

Huu ni mchezo wa tano wa kirafiki kwa Heroes kufuatia awali kutoka sare ya bao 1-1 na Kombain ya Unguja, kisha wakatoka tena sare ya 1-1 na Taifa ya Jang'ombe, wakaifunga Villa United 5-2, jana wakaichapa Dulla Boys 2-1 na leo kushinda 2-0.

Kwasasa Heroes watacheza mchezo mmoja tu wa kirafiki kabla ya kuelekea Kenya katika Mashindano ya CECAFA ambapo mchezo wao wa mwisho wa kujipima nguvu utapigwa siku ya Jumanne saa 11:00 za jioni katika uwanja wa Amaan dhidi ya Kombain ya Wachezaji wanaocheza ligi kuu soka Tanzania Bara ambao hawakuitwa Heroes.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE