CHINONSO APIGA HAT-TRICK CHARAWE WALIPOPIGWA NA CHUONI, MIEMBENI CITY JAMVI LA WAGENI

Mshambuliaji Charles Chinonso amefunga mabao matatu (Hat-trick) na kuiongoza Chuoni kuichakaza Charawe kwa mabao 4-0 kwenye mchezo wa ligi kuu soka ya Zanzibar Kanda ya Unguja uliopigwa jioni ya leo kwenye uwanja wa Amaan.

Chinonso amefunga mabao hayo katika dakika ya 9, 11 na 26 huku bao jengine likifungwa na Mustafa Zakaria dakika ya 49.

Mapema saa 8 za mchana timu ya Miembeni City ikaendelea rikodi yake mbovu ya kufungwa baada ya leo kufungwa 2-1 na Kipanga.

Mabao ya Kipanga yamefungwa na Imran Abdul dakika ya 8 na Said Salum dakika ya 32 na lile la Miembeni City limefungwa na Feisal Riambi dakika ya 18.

Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa kupigwa mchezo mmoja katika uwanja wa Amaan majira ya saa 10:00 za jioni kati ya Taifa ya Jang'ombe dhidi ya KVZ.

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS