KAMARA AWAPONGEZA WAAMUZI WA ZANZIBAR WALOPATA BEJI YA FIFA

Katibu wa Waamuzi wa Soka Zanzibar Muhsin Ali “Kamara” amewapongeza waamuzi wanne wa Zanzibar waliyopata beji ya FIFA.

Kamara amesema ni faraja kwa Zanzibar kutoa waamuzi wa nne wenye beji hiyo ya FIFA.

Jana Shirikisho la Kimataifa la Soka (FIFA), limetoa beji kwa Waamuzi 18 wa Tanzania kati yao wanne kutoka Zanzibar katika msimu wa mshindano mwaka 2018.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka FIFA, Waamuzi walioteuliwa kutoka Zanzibar ni Mfaume Ali akiwa ni Muamuzi wa kati huku Wasaidizi walipewa beji hizo Mgaza Kunduli, Mbaraka Haule na mwanamama Dalila Jaffari.

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS