RASMI MASHINDANO YA CHALENJI YASOGEZWA MBELE HADI DISEMBA, ZANZIBAR HEROES YAZIDI KUPIKWA

Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) limesogeza mbele Mashindano ya Kombe la Chalenji.

Mashindano hayo yalitarajiwa kuanza Novemba 25 hadi Disemba 9, 2017 lakini sasa yataanza Disemba 3 hadi 17, 2017 nchini Kenya.

Akizungumza na Mtandao huu Afisa Habari wa Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) Ali Bakar "Cheupe" ametoa taarifa kuhusu kupelekwa mbele Mashindano hayo.

"Tumepokea Barua kutoka CECAFA kuwa mashindano ya Chalenj yamesogezwa mbele mpaka Disemba 3 kwaiyo timu yetu itaendelea na mazoezi kujiandaa na mashindano hayo". Alisema Cheupe.

Jumla ya Mataifa 12 yanatarajiwa kushiriki Mashindano hayo wakiwemo wenyeji Kenya, Uganda, Somalia, Sudan, Ethiopia, Sudan ya Kusini, Burundi, Rwanda, Tanzania bara, Zanzibar, huku Libya na Zimbabwe zikialikwa kuchukua nafasi ya Djibouti na Eritrea.




Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE