ZANZIBAR HEROES LEO YAPOKEA MILIONI 5 KWA WAZALENDO WAWILI

Baadhi ya Wanamichezo wameshaanza kujitokeza kuichangia timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) ambayo inatarajiwa kwenda nchini Kenya kwenye Mashindano ya CECAFA Chalenj Cup.

Miongoni mwa wanamichezo hao waloanza kuichangia timu hiyo ni Mbunge wa Jimbo la Mpendae Salim Hassan Turky ambae amechangia Shilingi Milioni 3 pamoja na baadhi ya Vyakula kwaajili ya Kambi ya timu hiyo inayoanza rasmi Jumamosi.

Mbali ya Turky pia kampuni ya Ndege ya Assalam Air nayo imechangia Shilingi Milioni 2.

Kwa niaba ya Kampuni hiyo Ali Khatib Dai ametangaza kuchangia Milioni mbili ambapo amesema lengo lao ni kuwapa nguvu mashujaa hao wa Zanzibar.

Meneja wa timu ya Zanzibar Heroes Abdul wahab Haji Dau amewataka wanamichezo wengine kujitokeza kuichangia timu hiyo kwani bado hali yao si nzuri kifedha.

"Tunawashukuru hawa walioanza kuchangia leo, tunawaomba na Wadau wengine waichangie hii timu yao kwani bajeti yetu zaidi ya Shilingi milioni 80". Alisema Dau.
Turky alovaa nguo nyeupe baada ya kumpa Milioni 3 Meneja wa Heroes alovaa nyekundu

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE