ZANZIBAR HEROES WAENDELEA KUJIFUA, SELEMBE PEKEE KAFIKA KUTOKA LIGI KUU BARA


Ikiwa leo ni siku ya nane tangu kuanza mtizi Kikosi cha timu ya Taifa ya Soka ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) kinaendelea na mazoezi yake kujiandaa na Mashindano ya CECAFA Chalenj CUP yanayotarajiwa kufanyika Novemba 25 na kumalizika Disemba 9, 2017 huko nchini Kenya.

Mazoezi hayo yanayosimamiwa na kocha mkuu wa kikosi hicho Hemed Suleiman (Morocco) yanaendelea kila siku kuanzia saa 2:00 za asubuhi katika uwanja wa Amaan Mjini Unguja ambapo kocha huyo ametangaza kikosi cha awali cha wachezaji 30.

Mpaka sasa wachezaji waliyoanza mazoezi ni wale ambao vilabu vyao vya Unguja na Pemba huku ikiwa bado wachezaji wanaocheza ligi kuu soka Tanzania Bara hawajafika isipokuwa mmoja tu Suleiman Kassim (Seleembe) kiungo mshambuliaji wa Majimaji ya Songea.

Wachezaji waliyoanza mazoezi ni Walinda mlango Ahmed Ali "Salula" (Taifa ya Jang'ombe) na Mohammed Abdulrahman "Wawesha" (JKU), Nassor Mrisho (Okapi), Walinzi Mohd Othman Mmanga (Polisi), Ibrahimm Mohammed "Sangula"(Jang'ombe Boys), Abubakar Ame "Luiz" (Mlandege), Issa Haidar "Mwalala" (JKU) na Ibrahim Abdallah (Taifa ya Jang'ombe).

Viungo Abdul-swamad Kassim (Miembeni City), Abdul Aziz Makame (Taifa ya Jang'ombe), Amour Suleiman "Pwina" (JKU), Hamad Mshamata (Chuoni), Omar Juma "Zimbwe" (Chipukizi) na Mbarouk Marshed (Super Falcon) pamoja na washambuliaji Ali Badru (Taifa ya Jang'ombe), Salum Songoro (KVZ), Khamis Mussa "Rais" (Jang'ombe boys), Ibrahim Hamad Hilika (Zimamoto) pamoja na Mwalimu Mohd (Jamhuri).

Wachezaji ambao wanatokea ligi kuu soka Tanzania bara ambao bado hawajajumuika na wenzao ni Walinzi Abdallah Haji "Ninja" (Yanga), Adeyum Saleh "Machupa" (Kagera Sugar), Haji Mwinyi Ngwali (Yanga), Abdulla Kheir "Sebo" (Azam), Viungo Mudathir Yahya (Singida United), Mohd Issa "Banka" (Mtibwa Sugar) pamoja na washambuliaji Kassim Suleiman (Prisons), Matteo Anton (Yanga) na Seif Rashid Abdallah “Karihe” (Lipuli).

Kiungo mshambuliaji Feisal Salum (JKU) nae bado hajajiunga na wenzake kufuatia kuwepo kambi ya timu ya Taifa ya Vijana Tanzania wenye umri chini ya miaka 23 Kilimanjaro Warriors.
Suleiman Kassim (Seleembe)

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE