JKU KUCHEZA NA WAZAMBIA, ZIMAMOTO NA WA ETHIOPIA, YANGA NA SHELISHELI WAKATI SIMBA NA WA DJIBOUTI



Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) leo limetoa ratiba ya awali ya Kombe la Klabu Bingwa na Kombe la Shirikisho barani humo huku wawakilishi wa Zanzibar katika Mashindano hayo kuwajua wapinzani wao ambapo michezo ya awali yote wataanzia nyumbani Zanzibar katika uwanja wa Amaan.

JKU ambao ndio mabingwa watetezi wa Zanzibar wamepangwa kucheza na Zesco United ya Zambia kwenye Mashindano ya Klabu Bingwa huku Zimamoto ambao ni makamo Bingwa wa Zanzibar watacheza na Wolaitta Dicha ya Ethiopia.

Na kwa upande wa Wawilishi wa Tanzania bara katika Mashindano ya Klabu Bingwa, Yanga watacheza na St Louis ya Shelisheli huku Simba watakipiga na Gendamarie ya Djibouti kwenye kombe la Shirikisho.
 
Ibrahim Hamad Hilka mshambuliaji wa Zimamoto

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE