NYOTA WA 4 WA ZANZIBAR WAPIMWA MKOJO NA WORLD ANTI DOPING AGENCY KUHUSU KUTUMIA MADAWA YA KUONGEZA NGUVU

Mawakala wa kupinga utumiaji wa dawa za kuongeza nguvu Michezoni nchini kupitia tawi lao nchini Kenya (World Anti-Doping Agency “WADA”) kwa kushirikiana na Baraza la Vyama vya Michezo Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) linawasi wasi na  wachezaji wanne wa Timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) kutumia dawa hizo.

Wachezaji hao ni Kiungo Mohd Issa “Banka”, Fesal Salum “Fei Toto” na Washambuliaji Ibrahim Hamad Hilika na Suleiman Kassim “Seleembe”.

Hofu hiyo imekuja kwenye Mashindani ya Cecafa Senior Chalenj Cup jioni ya leo katika uwanja wa Kenyatta Mjini Machakos mara baada ya kutoka sare ya 0-0 na Wenyeji Kenya na kupelekea Zanzibar kutinga moja kwa moja nusu fainali wakiwa na alama 7 wakiongoza kundi lao A lenye Mataifa kama Kenya, Libya, Rwanda na Tanzania bara.

WADA na CECAFA wameingiwa na wasi wasi kutokana na kiwango bora walichoonyesha Zanzibar katika Mashindano hayo huku ikiwaongoza mataifa kama Libya, Rwanda, wenyeji Kenya na Tanzania Bara.

WADA na CECAFA baada ya kumaliza mchezo wa leo waliwafata wachezaji hao katika vyumba vya kubadilisha nguo lakini hawakufanikiwa kuwapima jambo ambalo limepelekea kuwafata mpaka kambini kwao kwenye Hoteli ya Garden iliyopo Mjini Machakos nchini Kenya.

Awali walisema Wachezaji wa Zanzibar wana mashaka nao na jinsi wanavyocheza si bure, hivyo baadae wakawataja wachezaji hao wanne akiwemo kiungo kinda Fesal Salum “Fei Toto” ambae leo amechaguliwa kuwa nyota wa mchezo wa leo kati ya Zanzibar na wenyeji Kenya ulomalizika 0-0.

Tangu kuanza Mashindano haya mwaka huu Zanzibar inaongoza kutoa wachezaji bora wa mchezo yani Men of the Match ambapo mchezo wa awali Zanzibar Heroes waliichapa Rwanda mabao 3-1 huku mchezaji bora akitajwa kuwa Mohd Issa “Banka”, mchezo wa pili Zanzibar waliwafunga Tanzania bara mabao 2-1 na mchezaji bora wa mchezo akawa Ibrahim Hamad “Hilika” na leo Zanzibar 0-0 Kenya mchezaji bora pia katoka Zanzibar Fesal Salum.

Hivyo wale wote nyota wa mchezo wa Zanzibar wameorodheshwa katika kundi hilo.

Kwasasa zoezi hilo la kupimwa mkojo kwa wachezaji hao linafanywa hapa Garden Hotel Machakos, endelea kufatilia Blog hii utajua zoezi hilo linavyokwenda.







Comments

  1. Ndio kawaida ya Waswahili wakikuona unaelekea kwenye mafanikio basi atakuekea kikwazo tu

    ReplyDelete
  2. Ndio kawaida ya Waswahili wakikuona unaelekea kwenye mafanikio basi atakuekea kikwazo tu

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE