SARE DHIDI YA LIBYA YAMSONONESHA ERASTO NYONI



 NAHODHA wa Timu ya Taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) Erasto Edward Nyoni anaonekana kusononeshwa na sare waliyotoka na Libya baada ya kusema kuwa walitegemea kushinda lakini haikuwa bahati kwao.

Katika mchezo huo wa jana, wa kombe la CECAFA SENIOR CHALLENGE CUP uliopigwa katika uwanja wa Kenyatta uliopo Machakos nchini Kenya, Kilimanjaro walipata kazi ngumu mbele ya Waarabu wa Libya na kulazimika mchezo huo kutoka sare ya 0-0.

“Tulitegemea kupata ushindi lakini imeshindikana, Libya ni wazuri lakini tunashkuru Mungu kupata alau hiyo point moja”. Alisema Nyoni.

Mchezo wa pili Kilimanjaro Stars itacheza na ndugu zao Zanzibar Heroes siku ya Alhamis ya Disemba 7 saa 8:00 za mchana katika uwanja wa Kenyatta .


Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE