ZANZIBAR HEROES IKIIFUNGA KENYA KESHO INATINGA NUSU FAINALI KWA KISHINDO



Timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) ndio kinara wa kundi lao A wakiwa na alama sita katika Mashindano ya kuwania ubingwa wa Kombe la Chalenji kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati (CECAFA SENIOR CHALLENGECUP) Mashindano ambayo yanaendelea nchini Kenya.

Mchezo wa awali Zanzibar Heroes iliichapa Rwanda mabao 3-1 kwa magoli yalofungwa na Mudathir Yahya, Mohd Issa (Banka) na Kassim Suleiman huku mchezo wa pili jana waliifunga Tanzania bara (Kilimanjaro Stars) mabao 2-1 kwa msaada wa mabao yalofungwa na Kassim Suleiman na Ibrahim Hamad Hilika ambapo kesho Jumamosi watacheza mchezo wa tatu dhidi ya wenyeji Kenya.

Endapo kesho Heroes wakifanikiwa kuwafunga Kenya watajihakikishia kutinga hatua ya nusu fainali kwani watafikisha alama 9, alama ambazo hazitoweza kufikiwa na timu yoyote katika kundi hilo.

Katika Mashindano ya mwaka huu Heroes inaonekana kuwavutia wapenzi wengi kutokana na soka safi wanalolitandaza na kuonyesha vipaji walivyonavyo, jambo ambalo limepelekea Wakenya wengi hapa Mjini Machakos kusema kuwa timu yao wanayoipenda ni Zanzibar.


Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE