ZANZIBAR YATINGA FAINALI MASHINDANO YA BEACH SOKA, YAONGOZA KULIKO NCHI ZOTE WATACHEZA TENA NA MALAWI FAINALI

Timu ya taifa ya Zanzibar ya soka la ufukweni (Zanzibar Sand Heroes) imefanikiwa kutinga fainali katika Mashindano ya Copa Dar es salam yanayoendelea katika Ufukwe wa Coco Jijini Dar es salam baada ya asubuhi ya leo kuwachapa Malawi mabao 5-1.

Mchezo mwengine leo Uganda wakaichapa Tanzania bara kwa mabao 6-5.

Kwa matokeo hayo Zanzibar imeongoza katika Mashindano hayo wakishika nafasi ya kwanza huku Malawi wamekamata nafasi ya Pili ambapo Tanzania bara wakishika nafasi ya tatu na Uganda wakikamata nafasi ya nne.

Hivyo fainali itachezwa na timu ilokamata nafasi ya kwanza (Zanzibar) dhidi ya timu iloshika nafasi ya pili (Malawi) huku mshindi wa tatu watachuana kati ya timu iloshika nafasi ya tatu (Tanzania Bara) na Uganda waliomalizia nafasi ya nne.


Michezo hiyo itapigwa jioni ya leo Jumanne katika fukwe za Coco ambapo utaanza kuchezwa mchezo wa kusaka mshindi wa tatu kisha kumalizwa fainali.

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS