JKU APIGWA 7-0 KOMBE LA KLABU BINGWA HUKU ZIMAMOTO AKIFA KIUME KOMBE LA SHIRIKISHO


Wawakilishi wa Zanzibar katika Mashindano ya klabu Bingwa na Kombe la Shirikisho Barani Afrika JKU na Zimamoto zote zimetolewa rasmi leo katika Mashindano hayo baada ya kufungwa ugenini katika michezo yake ya marejeano.

Katika kombe la Klabu Bingwa JKU wamefungwa na Wenyeji Zesco ya Zambia mabao 7-0 na kufanya kutelewa kwa jumla ya mabao 7-0 kufuatia mchezo wa awali uliochezwa Amaan Zanzibar kumalizika kwa sare ya 0-0.

Mabao ya Zesco manne yamefungwa  na Zikiru Adams dakika 4, 42, 57, 60 huku mengine yakifungwa na Lazarus Kambole dakika 36, Winston Kalengo dakika 77 na Lameck Banda dakika ya 87.

Kwa upande wa Zimamoto ambao walikuwa wanawakilisha Zanzibar katika Kombe la Shirikisho nao wametolewa kwa kufungwa 1-0 na wenyeji wao Wallaita Dicha ya Ethiopia na kufanya watolewe kwa jumla ya mabao 2-1.

Bao pekee la Wallaita Dicha limefungwa na Arafat Djako dakika ya 29.

Huu ni mfululizo wa kufanya vibaya kwa vilabu vya Zanzibar katika Mashindano hayo kufuatia msimu uliopita timu ya Zimamoto na KVZ zilitolewa katika hatua ya awali kwenye Mashindano hayo .

Kwenye klabu bingwa Zimamoto ilitolewa na timu ya Ferroviario Beira ya Msumbiji baada ya kufungwa mabao 3-1 katika mchezo wa mwisho wa ugenini ambapo awali nyumbani walishinda 2-1 hivyo wakatolewa kwa kufungwa jumla ya mabao 4-3.

Na kombe la Shirikisho timu ya KVZ nayo ilitolewa katika mashindano hayo baada ya kufungwa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Messager Ngozi ya Burundi baada ya mchezo wa mwanzo uliochezwa Zanzibar KVZ walishinda 2-1, hivyo walitolewa kwa kufungwa jumla ya mabao 4-2.


Wachezaji wa JKU kushoto Amour Suleiman (Pwina) na kulia Issa Haidar (Mwalala)

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS