NAGE (REDE) ZANZIBAR WAENDA DAR ES SALAM KUWAFUNDISHA WENZAO MCHEZO HUO

Wachezaji wa mchezo wa Nage Zanzibar wametakiwa kuukuza mchezo huo Tanzania bara ili kuiletea sifa Zanzibar katika Michezo.

Akizungumza wakati wa kuziaga timu nne za mchezo wa Nage Zanzibar Talib Ali Talib ambae ni mwenyekiti  wa CCM Mkoa wa mjini, amesema lengo la kwenda Tanzania bara ni kuukuza mchezo huo pia kuzidisha uhusiano wao na Tanzania bara katika kusheherekea miaka 41 ya kuzaliwa kwa chama cha CCM.

Timu nne za Nage zilizokwenda Jijini Dar es salam ni Miembeni Magic kutoka jimbo la Kikwajuni, karakana kutoka jimbo la Chumbuni, Six center kutoka Jimbo la Mwera na  yataka moyo kutoka jimbo la Welezo.
Kwa matokeo ya leo huko Dar es salam timu za Zanzibar zote zimeanza vyema ambapo Miembeni chupa 63-3 Magomeni ya Dar, Karakana City 45-15 Kinondoni ya Dar, Yataka moyo ya Welezo Zanzibar 17-8 Kijitonyama ya Dar.

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS