ZANZIBAR HEROES MAPEMA KUTANGAZWA NA KUANZA MAANDALIZI


Wizara ya Habari Utalii Utamaduni na Michezo imesema itahakikisha Chama cha soka Zanzibar (ZFA) inasimamia kufanya maandalizi ya timu ya taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) mapema mwaka huu ili izidi kutoa upinzani mkali katika mashindano ya Cecafa Senior Chalenj Cup.

Akijibu swali lililoulizwa na Mwakilishi wa Jimbo la Konde Omar Seif Abeid aliyetaka kujua wizara ina mpango gani kabambe uliondaliwa kuhakikisha Zanzibar Heroes inaendelea kutoa upinzani katika mashindano hayo, naibu waziri wa wizara hiyo Chum Kombo Khamis amesema wizara kwa kushirikiana na idara ya michezo itahakikisha kuwa ZFA inasimamia kufanyika maandalizi ya timu hiyo mapema ili kuleta ushindani katika mashindano hayo.

Zanzibar Heroes ilifanikiwa kushika nafasi ya pili katika mashindano ya Cecafa Senior Chalenj Cup mwaka jana baada ya kufungwa kwa penalty 3-2 na wenyeji Kenya kufuatia kutoka sare ya 2-2 ndani ya dakika 120.

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS