ZESCO UNITED YAWASILI ZANZIBAR, TAYARI KUWAVAA JKU JUMAMOSI


Wapinzani wa JKU katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika timu ya Zesco United kutoka Zambia wamewasili leo Zanzibar tayari kabisa kwa mchezo wa Jumamosi kwenye uwanja wa Amaan.
Timu hiyo imewasili leo saa nne asubuhi kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Aman Karume kwa ndege ya Shirika la Ndege la Kenya ambapo wachezaji wa timu hiyo wameongozana na viongozi wao na wamepokelewa na wenyeji wao ambao ni viongozi wa timu ya JKU.

Afisa habari wa chama cha soka Zanzibar (ZFA) Ali Bakar (Cheupe) amesema kwa upande wao Chama maandalizi yote wamekamilisha huku akiwataka Mashabiki wa soka kujitokeza kwa wingi kwenda kuzishangiria timu za Zanzibar.



Wawakilishi wa Zanzibar katika Mashindano hayo ya Kimataifa ni JKU ambao wataivaa Zesco United siku ya Jumamosi katika mchezo wa kombe la Klabu bingwa huku Zimamoto ambao watawakilisha kwenye kombe la Shirikisho wataivaa Walaitta Dicha ya Ethiopia siku ya Jumapili michezo yote itapigwa majira ya saa 10:00 za jioni katika uwanja wa Amaan.


Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS