KARUME BOYS WAKABIDHIWA BENDERA, TAYARI WAMESHAPANDA PIPA KWENDA BURUNDI KATIKA MASHINDANO YA CECAFA


Naibu Waziri wa Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo Lulu Msham amekabidhi bendera kwa timu ya taifa ya Zanzibar ya Vijana chini ya miaka 17 (Karume Boys) kwa ajili ya kushiriki michuano ya Cecafa ya Vijana nchini Burundi.

Hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Wizara ya Habari Utalii na Mambo ya Kale kikwajuni ambapo viongozi mbali mbali walihudhuria wakiwemo wa Wizara ya Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo, baraza la Taifa la michezo na chama cha soka ZFA.

Akitoa nasaha zake kwa wachezaji na viongozi wa timu hiyo Naibu Lulu amewataka wachezaji hao kujielewa wao ni nani na jukumu kubwa walilopewa na nchi yao huko wanakokwenda huku akiwasisitiza kudumisha nidhamu kwani ndio silaha yao.

Amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imewapa jukumu kubwa la kuiwakilisha nchi, hivyo lazima wafahamu majukumu yao na wanatakiwa kufanya ili kuhakikisha wanailetea sifa nzuri nchi yao pamoja na kuwa na nidhamu kubwa.

Mapema Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo Omar Hassan (King) amezitaja baadhi ya Taasisi zilizofanikisha safari ya Vijana hao wakiwemo Idara ya Uhamiaji Zanzibar, Wizara ya Afya pamoja na Hoteli ya Paradise International Hotel iliyotumika kwaajili ya kukaa Kambi timu hiyo kwa wiki tatu.

Kwa upande wake nahodha wa timu hiyo Ibrahim Ali Juma (Chafu) amewatoa hofu Wazanzibar na kusema wategemee Ubingwa kwani kikosi chake anakiamini mno.

Jumla ya msafara wa watu 29 wakiwemo Wachezaji 23, Makocha 2 na Viongozi 4 wameondoka Zanzibar leo kwa Ndege kwenda Burundi katika Mashindano hayo yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi lake April 14 hadi 28, 2018 ambapo Zanzibar imepangwa kundi ‘B’ pamoja na ndugu zao Tanzania bara, Sudan na Uganda huku kampeni zake Zanzibar kuwania kombe hilo zitaanza April 15 kwa kucheza na Sudan katika uwanja wa Gitega majira ya saa 7:30 za mchana.
Viongozi na Wachezaji wa Karume Boys wakisoma dua baada ya kuagwa



Comments

  1. Kiswandu tueleze kuhusu miaka y'a wachezaji wetu mana nimesikia tumefungiwa napia kulipishwa fain juu ya jambo miaka

    ReplyDelete
  2. Kiswandu tueleze kuhusu miaka y'a wachezaji wetu mana nimesikia tumefungiwa napia kulipishwa fain juu ya jambo miaka

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS