KOCHA MUU NAE AUTAKA URAIS WA ZFA, IDADI INAZIDI KUONGEZEKA


Kocha wa zamani wa timu ya Taifa ya Zanzibar ya Wanawake (Zanzibar Queens), Mtende Renger na Chuoni Mustafa Hassan (Kocha Muu) nae ametangaza nia ya kugombea Urais wa Chama cha Soka Visiwani Zanzibar (ZFA).

Amesema kwa vile analijua vyema soka la Zanzibar na uzoefu wa kuongoza anao ameona ipo haja kuongoza Chama hicho.

Kocha Muu atafanya idadi ya Wadau wa soka kuongezeka walotangaza nia ya kugombea nafasi hiyo baada ya hivi karibuni Mwakilishi wa jimbo la Uzini Mohammedraza Hassanal, Abdul Hamid Mshangama na kocha wa Zamani wa timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) Salum Bausi wote kutangaza nia ya kugombea nafasi hiyo katika uchaguzi mdogo unaokuja.

ZFA watalazimika kufanya uchaguzi kufuatia viongozi wake wakuu kuamua kujiuzulu akiwemo aliyekuwa Rais Ravia Idarous Faina, Makamo Urais ZFA Pemba Ali Mohammed Ali na Makamo Urais ZFA Unguja Mzee Zam Ali hivyo nafasi hizo mpaka sasa zipo tupu huku ikisubiriwa kamati ya Uchaguzi kutangaza tarehe za kuanza harakati za kufanyika uchaguzi huo.

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS