WASOMALI WANAOCHEZA NA MALINDI CAF WAMEOMBA MECHI ZAO ZOTE KUCHEZWA ZANZIBAR


Wapinzani wa timu ya Malindi ya Zanzibar kwenye Mashindano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika timu ya Mogadishu City Club (MCC) kutoka Somalia wameliomba Shirikisho la Soka Zanzibar (ZFF) michezo yao yote miwili wa nyumbani na ugenini ichezwe Zanzibar.

Mchezo huo utachezwa Jumapili Agost 11, 2019 kwenye uwanja wa Amaan majira ya saa 10:00 za jioni ambapo MCC licha yakucheza ugenini (Amaan) itakuwa ndio mwenyeji wa mchezo huo wa kwanza.

Katika kujiandaa na mchezo huo dhidi ya Malindi MCC leo watacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya FC Heegan kwenye uwanja wa Benadir majira ya saa 10:00 za jioni.

Timu hiyo itasafiri kutoka Somalia kwenda Zanzibar Agost 7, 2019 ambapo MCC inawakilisha Somalia kwenye Mashindano hayo baada kuifunga kwa penalty HorseedSC 4-3 kwenye kombe la Daa (FA CUP) kufuatia kwenda sare ya 0-0 ndani ya dakika 90 ambapo na Malindi wamepata nafasi hiyo baada ya kuichapa JKU kwa Penalty 4-3 kufuatia dakika 120 kutoka sare ya 0-0 kwenye mchezo wa fainali wa kombe la FA.

Timu ya Mogadishu City Club (MCC) imeanzishwa mwaka 1963 kwa msaada wa Meya wa mji mkuu wa Mogadishu ambapo mbali ya Soka pia inamiliki timu za michezo mengine kama vile timu ya mpira wa kikapu, Timu ya mpira wa mikono, Timu ya mpira wa meza, timu ya Lawn tenisi, timu ya mpira wa wavu, Timu ya kuogelea, timu ya riadha na timu ya Baskeli.

Wawakilishi wengine wa Zanzibar kwenye Mashindano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika timu ya KMKM watakuwa na kazi kucheza na Deportivo de Agosto ya Angola mchezo ambao utasukumwa Agost 10, 2019 saa 10:00 za jioni kwenye uwanja wa Amaan.


Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS