ZANZIBAR IMEPANGWA TENA KUNDI MOJA NA TANZANIA BARA CECAFA


Timu ya Taifa ya Vijana ya Zanzibar U-20 imepangwa kundi moja na ndugu zao Tanzania bara kwenye Mashindano ya Vijana ya Cecafa U-20 inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi rasmi Septemba 21, 2019 huko Uganda.

Timu hizo zimepangwa kundi B pamoja na Kenya na Ethiopia ambapo kundi A wamo wenyeji Uganda, Eritrea, Djibouti na Sudan huku Burundi ikipangwa kundi C pamoja na Sudan ya Kusini na Somalia.

Baada ya Zanzibar na Tanzania Bara kupangwa kundi moja Watanzania wengi watayakumbuka Mashindano ya Cecafa Senior Chalenj Cup mwaka 2017 huko Machakos nchini Kenya ambapo pia walipangwa kundi moja na Zanzibar ikawachapa Tanzania bara mabao 2-1.


Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS